• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

MAMBO KUMI NA MOJA (11) YANAYOCHANGIA NA KUONGEZA UWEZEKANO WA MTU KUPATA SARATANI YA MATITI

 Saratani ya matiti n moja ya saratani ambazo zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa kudhoofisha afya pamoja na kupelekea vifo miongoni mwa wanawake wengi duniani. Kwa Tanzania saratani hii hushika nafasi ya pili baada ya saratani ya shingo ya uzazi kwa kusababisha vifo miongoni mwa wagonjwa wenye saratani mbalimbali. Inakadiriwa mpaka kufikia mwaka 2030, idadi ya waathirika itakuwa imefika mpaka 82% hivyo ni muhimu sana kwa watu kufahamu mambo ambayo ni hatarishi na kuweza kuchukua tahadhari mapema. Mambo haya yanayochangia ni pamoja na; 

1. Kuongezeka umri
-Hii ni sababu ambayo ni kubwa na haiwezekana kuizuia. Kadiri umri unavyoongezekana tangu kuzaliwa ndio nafasi ya kupata saratani hii nayo huongezeka. 
-Tafiti nyingi zimeonesha kuwa wanawake wengi wanakuwa kwenye nafasi kubwa ya kupata saratani hii katika umri wa miaka 40 hadi 60.
-Hivyo ni muhimu kufanya uchunguzi wa matiti inapofika umri wa miaka 40 na kuendelea ili kuweza kujua afya yako mapema.
2. Jinsi ya kike
-Kuwa mwanamke ni kihatarishi cha moja kwa moja kwani imeonakena kuwa saratani hii ya matiti huwaathiri wanawake mara 100 za wanaume. 
-Kitu cha kukumbuka hapa ni kuwa hata wanaume wanaweza kupata saratani hii ingawa tu nafasi ya wanaume ni ndogo
3.Asili ya watu weupe(wazungu).
-Tafiti mbalimbali zimeonesha kuwa asili ya watu weupe wamekuwa katika nafasi kubwa ya kupatwa na saratani hii ukilinganisha na watu wenye asili ya weusi.
-Hii haina maana kuwa watu weusi hawapati, wanapata saratani hii pia lakini katika kiwango tofauti kidogo na watu wenye asili ya weupe (wazungu)
4. Historia ya saratani katika familia.

-Uwepo wa historia ya saratani ya matiti miongoni mwa wanafamilia kama baba, mama au watoto huongeza nafasi kubwa kwa mtu mwingine kupata saratani hii kwa baadae.

-Kadiri idadi ya waathirika katika familia inavyokuwa kubwa ndio na nafasi ya kupata saratani ya matiti inaongezeka.

-Mbali na historia ya saratani ya matiti, kuna historia ya saratani ya ovari nayo huongeza nafasi ya mwanafamilia kuathirika na saratani ya matiti

5. Historia binafsi ya saratani au maradhi ya titi ambayo si saratani.

-Mwanamke ambaye ana historia ya saratani ya titi wakati fulani anakuwa katika uwezekano mkubwa na kupata tena saratani hii miaka ya mbeleni katika titi lile lile au jingine.

-Lakini pia kuna maradhi ya matiti ambayo si saratani mwanamke anaweza akawa nayo yakamuongezeka nafasi ya kupata saratani ya matiti kwa miaka ya mbeleni.


6. Kupata hedhi ya kwanza katika umri mdogo au kuchelewa kufunga mzunguko.

-Tafiti nyingi zimeonesha kuwa kupata hedhi ya kwanza katika umri mdogo hasa kabla ya miaka 13 huweza kuchangia kwa saratani hii baadae ukilingani na kupata hedhi ya kwanza baada ya miaka 15.

-Suala hili limekuwa likihusishwa na athari ya muda mrefu ya homoni ya estrogeni kwa makundi haya mawili.

7. Mwili kupata tiba mionzi kabla ya miaka 30.

-Kupata tiba inayohusisha mionzi hasa katika maeneo ya kifua na hata matiti kutoka na sababu zingine za kiafya huweza kuchangia kutokea kwa saratani hii.

-Hii hutokana na uwezekano wa mionzi hiyo mikali na yenye nguvu kuathiri seli ya mwili katika eneo husika.

8. Kuchelewa kupata ujauzito wa kwanza au kutozaa kabisa.

-Kutozaa au kuchelewa kupata ujauzito katika umri mkubwa hasa kuanzia miaka 35 na kuendelea huongeza uwezekana wa kupata saratani ya matiti.

-Kuzaa kumeonekana kuwa na msaada kwa kipindi dhidi ya saratani ya matiti.  

-Suala hili huenda sambamba na kutonyonyesha wa mtoto ambapo huongeza nafasi ya saratani hii.

9.  Matumizi ya madawa ya uzazi 

-Dawa za uzazi wa mpango za kumeza ambazo ndani yake huwa na homoni ya estrogeni huchangia kutokea kwa saratani hii ikiwa zitatumika kwa zaidia ya miaka mitano

-Matumizi ya dawa za homoni (estrogeni na progesteroni) kwa akina mama baada ya kufunga mzunguko ni hatari kwani kuweza kupelekea saratani ya matiti pia.

10. Unene 

-Mbali na vihatarishi vingine, nafasi ya kupata saratani ya matiti imeonekana kuongezeka miongoni mwa wanaake ambao ni wa nene ukilinganisha na ambao wako kwenye uzito wa kawaida.

-Jambo hili limeonekana likiathiri zaidi wanawake ambao wamefunga mzunguko wa hedhi huku uzito wa kawaida kwa wanawake ambao bado hawajafunga mzunguko huwapunguzia nafasi ya saratani hii.

11. Utumiaji wa pombe na sigara

-Matumizi ya vitu hivi huchangia kwa wanawake wengi kuathirika na saratani hii ya matiti na hapa ni aidha unatumia kimoja wapo au vyote bado uwezekano upo pale pale kuliko ambaye hatumii kabisa.

Ufahamu wa mambo haya hatarishi kwa saratani ya matiti ni muhimu kwani unaweza ukafanya tathimini mwenyewe na kujua wapi pa kurekebisha hasa kwa mambo ambayo yanaweza kudhibitika. Kwa kufanya hivi basi unapata nafasi ya kuendelea kujiwekea mazingira salama kwa afya bora. 

Share:

NAMNA MGONJWA WA KISUKARI ANAVYOWEZA KUEPUKANA NA UPOFU KUTOKA NA UGONJWA HUO

 Ugonjwa wa kisukari huathiri takribani mifumo yote mwili huku macho yakiwa ni moja ya viungo ambavyo huathiriwa sana na sukari. Uwezekano wa macho ya mgonjwa mwenye kisukari kuathiriwa ni mara 25 zaidi ya mtu asiye na kisukari. Matatizo ya macho kwa mgonjwa mwenye kisukari yanaweza kuwa ya kupungua uwezo wa kuona (kuona ukungu ukungu) hadi kushindwa kuona kabisa (upofu). Sehemu mbalimbali katika jicho huathirika zikiwemo lensi ya jicho, mishipa ya damu kwenye jicho n.k

Baadhi ya mambo ya kuzingatia ili kuweza kuepusha macho yako kutokana na ugonjwa huu ni 

1.Kudhibiti kiwango chako cha sukari kwenye damu.

-Hili ni jambo la kwanza na la muhimu kabisa kulifanya ili usipatwe na maradhi haya ya macho. Kufanikisha udhibiti wa sukari mwili ni pamoja na ;

  • Kuzingatia mtindo bora wa maisha yani kufanya mazoezi kila siku inavyoshuriwa, kuzingatia taratibu za ulaji wa chakula, kuepuka sigara na pombe
  • Kutumia dawa za ugonjwa wa kisukari kadiri ya maelekezo ya daktari 
2. Kudhibiti shinikizo la juu la damu

-Shinikizo la juu la damu pamoja na ugonjwa wa kisukari ni matatizo ambayo huwa yanaendana kwa karibu sana huku ugonjwa wa kisukari ukiwa ni kihatarishi kikubwa cha tatizo la shinikizo la juu la damu.

-Matatizo haya yote mawili kwa pamoja huathiri mishipa ya damu katika jicho na hivyo kufanya athari kuwa kubwa zaidi na kushamiri kwa haraka zaidi.

-Mgonjwa mwenye Kisukari anatakiwa kudhibiti kiwango chake cha shinikizo la damu kwa kiasi cha milimita za Mekyuri 130/80 au chini ya hapo ili kuwa katika mazingira salama zaidi.

3. Kuzingatia uchunguzi wa macho kadiri inavyotakiwa.

-Mgonjwa wa kisukari ni muhimu sana kufanya uchunguzi wa macho kila baada ya muda flani kwani kwa kufanya hivi husaidia kugundua hali ya jicho mapema kama tatizo limeshaanza au la na kujua hatua ya kufanya.

  • Fanya uchunguzi wa macho mara moja kila mwaka endapo tu udhibiti wa sukari uko vizuri kama inavyotakiwa
  • Fanya uchunguzi wa macho angalau kila baada ya miezi 3-6 endapo udhibiti wa sukari ni hafifu
  • Fanya uchunguzi wa macho angalau kila baada ya miezi 6 endapo tayari kuna athari kidogo ya macho kutokana na sukari + udhibiti wa sukari unaenda vizuri.
4. Kupata matibabu ya macho mapema.

-Tiba ya mapema ya macho endapo kuna hitilaju tayari husaidia katika kuboresha uwezo wa macho kuona lakizi pia husaida katika kupunguza kuendelea kwa madhara zaidi. 

-Kuchelewa kwa matibabu ya macho katika hatua za awali ni hatari kwani taratibu unaweza kupatwa na upofu kabisa.

-Fika katika hospitali na uweze kuonana na wataalamu wa macho kwa tiba sahihi.

Kisukari bila upofu inawezekana, suala la msingi ni kuzingatia mambo yote yaliyoelezewa na pia kujenga utamaduni wa kuonana na mtaalamu wa afya kwa ushauri zaidi. Unapoona utofauti wa uonaji wako usisite kufika hospitalini mara moja.



Share:

ZINGATIA HIZI KANUNI NNE (4) KATIKA PROGRAMU YOYOTE YA MAZOEZI UNAYOTAKA KUANZA ILI UPATE MATOKEO SAHIHI.

Ni muhumi sana kila unapotaka kuanza mazoezi uwe umejiwekea malengo kadhaa ya kupata baada ya kipindi fulani cha mazoezi. Moja ya lengo la watu wengi katika mazoezi ni kuwa fiti au imara ingawa mambo mambalimbali huchangia katika utofauti wa matokeo haya miongoni mwa watu kama vile umri, jnsi, vinasaba, lishe n.k. Kama mwanamazoezi ni muhimu kutambua kuwa ili kufikisha malengo yako ni lazima uweze kufuata kanuni hizi katika programu yako ya mazoezi, kanuni hizo ni 

1. Fanya aina hususani ya mazoezi. (Specificity)
-Kila unapofanya mazoezi ni vema kulenga mazoezi moja kwa moja yanakupatia matokeo husika na si vinginevyo.
- Kama uko katika darasa la mazoezi na unataka kufanya mazoezi ya kuimarisha mfumo wa moyo na pumzi basi inatakiwa ujikite moja kwa moja katika mazoezi ya aerobiki ndani ya muda fulani.

 -Na kama unataka kujenga misuli basi ni vyema ukafanya mazoezi husika moja kwa moja (pushups, kunyanyua vyuma n.k) na ukaenda zaidi katika kila misuli na muda wake.

-Kanuni hii husaidia sana kupata matokeo kwa uhakika zaidi na ndani ya muda mfupi kuliko kuwa na tabia ya kuchanganyachanganya mazoezi ambacho ndio kinafanywa na watu wengi. Tabia kama hii imewafanya watu wengi kutopata matokeo sahihi.
2. Fanyisha mwili mazoezi kuliko kawaida yake. (Overload)
-Kila mara unapofanya mazoezi ni lazima kuongeza jitihada ya kuufanyisha mwili zaidi na zaidi kuliko wakati kawaida yake kwani mwili hubadilika kila siku kulingana na uzito wa kazi unavyoongezeka ili kwenda sambamba.

-Mifupa huwa imara zaidi unapotembea umbali mrefu zaidi na hata unapoubebesha vitu vizito kuliko mwili ukiwa haufanyi chochote na vilevile mfumo wa moyo, mapafu na mishipa ya damu huimarika zaidi unapokimbia umbali mrefu zaidi kuliko kukimbia umbali mfupi au kutokimbia kabisa.

-Kama unanyanyua vyuma basi ni vyema kujitahidi kuongeza namba ya "Reps" au "Sets" au uzito ili kuupa shuruba mwili na hivyo kuwa imara taratibu.
-Kuna watu ndani ya mwaka mzima wao hukimbia kilomita 1 au kama ananyanyua vyuma basi wao ni kilo 20 tu siku zote, hii si sawa kabisa kwa matokeo bora ya mazoezi.

3. Fanyisha mwili mazoezi zaidi leo kuliko jana.(Progression)
-Ni muhimu sana kuwa na namna bora ya kuweza kuufanyisha mwili mazoezi kuliko kawaida yake ili kupata matokeo mazuri zaidi. 

-Kadiri unavyoufanyisha mwili mazoezi fulani hufikia hatua huzoea mazoezi hayo hivyo kuna haja ya kuwa na muendeleo chanya katika maeneo ya idadi ya vipindi vya mazoezi, aina ya mazoezi na muda kwa ujumla vipindi vya mazoezi  husika.

-Kama leo umekimbia kilomita 1 basi kesho nenda asilimia 10 zaidi ya jana kisha kesho kutwa ongeza 10% zaidi hivyo hivyo, hapo mwili utaimarika na kukufanya uwe fiti.
4. Tenga siku za kupumzika
-Mapumzisho ya mwili ni sehemu muhimu sana katika mazoezi kwani husaidi mwili kujengeka na kurudisha nguvu iliyopotea katika vipindi vya mazoezi yalipita.
-Baadhi ya vigezo vya kuzingatia katika mapumziko ni pamoja na umri, hali ya hewa na aina ya mazoezi
  • Vijana zaidi ya miaka 25 wanahitaji muda mwingi wa kupumzika baada ya mazoezi
  • Mazoezi katika hali ya joto kali huhitaji pia muda mwingi wa mapumziko 
-Kwa mazoezi ambayo yanahusisha kurarua misuli kwa kunyanyua vyuma vizito sana basi angalau masaa 24 mpaka 48 ya kupumzisha misuli husika inafaa zaidi.

-Katika kipindi hiki ni muhimu kupata usingizi wa kutosha angalau masaa 7-8, kupata mlo kamili na maji ya kutosha huku ukiepuka matumizi ya sigara, pombe, na madawa yasiyofaa kama steroids.

-Kufanya mazoezi kila siku bila ya kupumzika huambatana na madhara mengi ikiwepo kupata athari za kujiumiza, mwili kutopata nafasi ya kujijenga na hivyo kutopata matokeo sahihi.


Kanuni hizi ni kubwa mno katika mazoezi na zinaweza kukuleta mabadiliko unayoyahitaji endapo tu utaweka utayapenda mazoezi, utaweka jitihada na kuwa mvumilivu katika kipindi chote cha mazoezi. Jitahidi kufikia malengo yako ya mazoezi na kuweza kudumisha malengo hayo kila siku. Ukiacha mazoezi nayo yatakuacha
Share:

ANDAA MLO KAMILI KWA KUCHAGUA ANGALAU CHAKULA KIMOJA KUTOKA KWENYE MAKUNDI HAYA MATANO (5) YA VYAKULA.

 Mlo kamili  ni ule ambao hutokana na chakula mchanganyiko kutoka katika makundi yote ya chakula na una virutubishi vyote muhimu kwa ajili ya lishe na afya bora. Ili kupata mlo kamili inafaa kuchangua angalau chakula kimoja katika kila kundi, hii husaidia moja kwa moja kupata virutubisho vyote mwilini.  Makundi haya huusisha vyakula mbalimbali ambayo huwa na virutubisho husika katika kila kundi, makundi hayo ;

1. Nafaka

-Hili ni kundi la chakula ambalo hujumuisha ngano, mchele, shayairi, mahindi, mtama n.k

-Vyakula hivi vya nafaka vinaweza kutumika moja kwa moja au kusagwa na kutumika kuandalia vyakula vingine kama chapati, maandazi, tambi, mkate, keki, biskuti , ugali , wali n.k

-Nafaka bora kiafaya siku zote ni zile ambazo hazijakobolewa kwani hubaki na virutubisho muhimu sana kuliko nafaka zilizokobolewa.

-Nafaka zisizokobolewa huwa na wingi wa makapi-mlo,vitamini na madini ambayo hayapatikani kwenye nafaka iliyokobolewa.

-Hivyo nafaka iliyokobolewa ni muhimu kuiongezea virutubisho.


 2. Mboga za majani

-Hili ni kundi kubwa la jamii ya aina mbalimbali za mboga za majani. Vyakula katika kundi hili vinatoka katika sehemu tofauti tofauti za mmea kama vile kwenye maji, shina, mbegu na mizizi

-Ni kweli kabisa tafiti zimeonesha ulaji wa mboga za majani kila siku huzuia magonjwa sugu yasiyoambukizwa kama saratani, kisukari n.k

-Baadhi ya makundi ya mboga za majani ni pamoja na;

  • Mboga zenye majani ya kijana; spinach, brocolli, kabeji, mchicha n.k
  • Mboga zenye majani mekundu na njano; karoti, nyanya,maboga, pilipili n.k
  • Mboga jamii ya kunde; njegere, maharagwe; kunde, dengu, jugu mawe
  • Mboga za jamii ya mizizi;Vitunguu, Bieetroot, tangawizi, karoti

3. Matunda
-Kuna matunda ya aina mbalimbali ambayo huweza kutumika yenyewe baada ya kukomaa au kuiva pia yanaweza kutumika katika utengenezaji wa juisi
-Matunda huwa na rangi tofauti tofauti , kula matunda ya rangi tofauti tofauti kwani husaidia kukupa virutubisho mbalimbali na hivyo kujenga vyema afya yako.
4. Vyakula vya protini
-Hili ni lundi la vyakula vyote vyenye virutubisho vya protini. Mbali na kuwa chanzo kizuri za protini, vyakula hivi huwa na virutubisho vingine kama madini zinki, chuma, vitamini na mafuta.
-Baadhi ya vyakula hivyo ni pamoja na;
  • Nyama -Inaweza kuwa ya ng'ombe, mbuzi, kuku n.k
  • Samaki na jamii ya vyakula vya majini- Pweza, kaa, prawn n.k
  • Mayai
  • Karanga na mbegu
  • Mboga jamii ya kund-Kundi hili huingia pia kwenye mboga za majani kwani huwa na virutubisho sawa na nyama, kuku samaki,na mayai.    

5. Maziwa na bidhaa zake
-Kundi hili hujumusiha maziwa na aina nyingine za vyakula zitokanazo na maziwa haya. 
-Maziwa yanaweza kuwa fresh, kukaushwa n.k na hivyo kupelekea bidhaa zingine kama mtindi na siagi.
Ni muhimu katika mlo wako kuchanganya vyakula kutoka katika makundi hayo yote ili kuweza kunufaika na virutubisho mbalimbali. Sahani lako linatakiwa kuwa na angalau chakula kimoja wapo bila ya kusahau maji safi na salama ya kunywa.

Share:

NJIA KUMI NA MOJA (11) MUHIMU ZA KUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUPATWA NA UGONJWA WA KIHARUSI

 Kiharusi ni moja ya tatizo kubwa ambalo huathiri watu wengi kwa kusababisha ulemavu na hata vifo duniani kote. Kutokana na ukubwa wa tatizo hili ni vyema kupata ufahamu wa njia mbalimbali za kupunguza nafasi ya kushambuliwa na ugonjwa huu wa kiharusi kwani masuala mengi yako ndani ya uwezo wa mtu na machache sana yako nje ya uwezo wa mtu ikiwemo umri, jinsi, asili au chimbuko la mtu pamoja na historia ya familia ya ugonjwa wa kiharusi.

1. Dhibiti shinikizo la juu la damu

-Hili ni suala la muhimu sana kwani ndio linaongoza kwa kuhatarisha tatizo la kiharusi miongoni mwa watu wengi. 

-Shinikizo la juu la damu huathiri mishipa ya damu na hivyo kusababisha athari katika mzunguko wa damu katika ubongo

-Tumia dawa za shinikizo la juu la damu kama inavyotakiwa huku ukifuata mtindo bora wa maisha. Usiache dawa za presha bila ushauri kutoka kwa daktari

2. Dhibiti ugonjwa wa kisukari

-Ugonjwa huu unachangia kwa kiasi kikubwa pia katika kupelekea ugonjwa wa kiharusi kutokana na athari yake katika mishipa ya damu.

-Endapo una ugonjwa huu basi ni vyema kutumia dawa za kisukari kama umeshaanza na kufuata mtindo bora wa maisha. Usiache dawa za kisukari bila ya ushauri kutoka kwa daktari

3. Acha kuvuta sigara

-Kemikali mbalimbali zilizomo katika moshi wa sigara huathiri moja kwa moja mfumo wa moyo pamoja na mishipa ya damu na hivyo kupalilia njia kwa ugonjwa wa kiharusi kutokea.

-Kuacha uvutaji wa sigara ni maamuzi sahihi kwa hukupunguzia nafasi ya kupatwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa.

4. Epuka vyakula vyenye mafuta mengi.

- Mafuta hasa kutoka kwenye jamii ya wanyama si mazuri kwa afya ya mwili hasa kwa mfumo wa moyo na mishipa ya damu kwani mafuta hayo huwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) mbaya .

- Cholesterol hii huweza kupelekea kwa utando katika mishipa ya damu na kuathiri mtiririko wa damu.

-Jikite zaidi katika mlo wenye mboga za majani kwa wingi, matunda, nafaka isiyokobolewa, mboga jamii ya kunde, maziwa na mazao yake 

-Punguza ulaji wa nyama, maini , vyakula vya kukaangwa kwenye mafuta mengi pamoja na vitu vyenye sukari nyingi.

5. Kupunguza kiwango cha chumvi katika mlo.

-Kitaalamu inashauriwa kutumia chumvi kiasi cha kijiko kimoja cha chai kwa siku katika milo tofauti tofauti ili kuwa salama zaidi. 

-Chumvi nyingi huathiri shinikizo la damu na hivyo huweza kupelekea kuwa juu na kusababisha kiharusi 

-Jenga tabia ya kutumia chumvi kidogo mno kwenye mlo.

6. Punguza uzito wako 

-Kama una uzito uliopitiliza au unene basi ni wakati sahihi wa kupunguza uzito huo na kisha kuudhibiti katika kiwango sahihi kiafya.

-Unene huathiri shinikizo la damu, huathiri udhibiti wa kiwango cha sukari mwilini na hata kuathiri moyo. Yote haya kwa pamoja ni hatari kwa ugonjwa wa kiharusi.

-Fanya mazoezi na kula mlo bora ili kudhibiti kiwango cha uzito mwilini.

7. Fanya mazoezi inavyotakiwa.

-Ni muhimu kufanya mazoezi kwa siku nyingi katika wiki kulingana na jinsi, umri, kazi na afya ya mtu kwa ujumla kwani mazoezi hukusaidia katika kuepukana na magonjwa sugu yasiyoambukiza.

-Fanya mazoezi angalau dk 30 kwa siku na zaidi onana na daktari ili pia kujua afya yako kabla ya mazoezi

8. Epuka au punguza unyaji wa pombe kupita kiasi

-Pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya ya mwili mwako kutoka na ukweli kuwa pombe huathiri mifumo mingi katika mwili ikiwemo mfumo wa moyo na mishipa ya damu, 

-Unywaji wa pombe unaweza kupelekea kutanuka kwa moyo ambapo ni hatari kwa ugonjwa wa kiharusi n.k

-Unywaji wa pombe wa wastani unaotakiwa kwa siku ni uniti 1 au chini kwa mwanamke na uniti 2 au chini kwa mwanaume. Ujazo na asilimia ya pombe katika chupa ndio husaidia kujua kiwango cha uniti 1 

9. Epuka matumizi horera ya madawa

-Matumizi ya baadhi ya madawa huweza kupelekea tatizo la kiharusi kwani huwa na athari katika mfumo wa damu na mishipa yake, madawa kama warfarin, cocaine n.k

-Kabla ya kutumia dawa yoyote ni muhimu kuwasiliana  na daktari kwa maelezo zaidi.

10. Fanya uchunguzi  endapo una maradhi ya moyo au selimundu.

-Endapo umegundulika kuwa na magonjwa ya moyo kama vile moyo kutanuka, mapigo ya moyo kutoenda sawa pamoja na maradhi ya selimundu basi ni muhimu kuwa na uchunguzi wa mara kwa mara kulingana na maelezo ya daktari

-Maradhi haya huchangia kwa kiasi kikubwa kupatwa kwa ugonjwa wa kiharusi endapo tahadhari zisipochukuliwa mapema.Hivyo kwa kufanya uchunguzi itakuwa ni rahisi kujua mwenedo wa maradhi haya na nini kifanyike katika kuboresha zaidi



11. Usiache kutumia dawa kama una historia ya kupata ugonjwa wa kiharusi

-Kama umewahi kupatwa na ugonjwa kiharusi basi ni vyema kuendelea kutumia dawa ulizoandikiwa na daktari kwani ni muhimu sana katika kuzuia kupatwa na kiharusi kwa mara nyingine.

-Usifanya maamuzi ya kuacha dawa mwenyewe mpaka pale utakaposhauriana na daktari.

Kwa kuzingatia njia hizi tofauti tofauti ni wazi kuwa kutapunguza kwa kiasi kikubwa kutokea kwa ugonjwa huu wa kiharusi. Utekelezaji unawezekana ukiamua kwa afya yako ni mtaji

Share:

WAKATI GANI DAWA(SINDANO) YA INSULINI HUTUMIKA KWA MGONJWA WA KISUKARI?

Insulini ni moja ya dawa muhimu sana katika matibabu ya ugonjwa wa kisukari kwani imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa wagonjwa wa kisukari katika kudhibiti sukari yao pamoja na kupunguza kasi ya madhara ya ugonjwa wa kisukari. Mbali na umuhimu huu wa Insulini bado baadhi ya wagonjwa wamesita kutumia dawa hii kutokana sababu mbalimbali ikiwemo; hofu ya kuchoma sindano, madhara kama ya kushusha sukari chini mno na uzito kuongezeka pamoja lakini kuwa na dhana potofu kuhusiana na dawa hii kama vile; matumizi ya kudumu ya insulini, ugonjwa kuwa mkubwa sana, uzembe binafsi wa kutodhibiti sukari vizuri kwa njia nyingine n.k.  
Dawa (sindano) ya Insulini imekuwa ikitumika katika hali mbalimbali kwa mgonjwa wa kisukari na hii yote ikiwa ni kufanikisha kiwango stahiki cha sukari mwilini, dawa hii hutumika kwa;

1. Mgonjwa wa kisukari aina ya kwanza (I)
-Wagonjwa wote wenye aina hii ya kisukari hutegemea sindano ya insulini katika kudhibiti sukari yako kwani kongosho yao haizalishi kabisa hompni ya Insulini. Hivyo wagonjwa hawa hutumia sindano hii siku zote katika maisha yao huku wakiendelea kufuata mtindo bola wa maisha.
Kwa wagonjwa wenye kisukari aina ya pili, sindano ya Insulini hutumika endapo;

2. Kushindwa kudhibiti sukari kwa kutumia dawa za kumeza
-Inapotokea dawa za kumeza zaidi ya moja katika dozi za kiwango cha juu kabisa zinashindwa kudhibiti kiwango cha sukari katika damu kwa muda wa miezi 2 had 3, inashauri kuanzisha sindano ya Insulini. 
-Hii husaidia kumuepusha mgonjwa huyu katika kipindi kirefu cha sukari ya juu ambapo anaweza kuanza kupata madhara zaidi.
3. Hali ya mgonjwa isiyomruhusu dawa za kumeza
-Kutoka na tathmini kutoka kwa daktari mgonjwa anaweza asiruhusiwe kutumia dawa za kumeza na akatakiwa kutumia sindano ya Insulini.
-Inawezekana mgonjwa akawa na hali zisizomruhusu kutumia dawa za kumeza kama; uzio (allergy) ya dawa, madhara makali ya dawa, maradhi makubwa kama figo kushindwa kufanya kazi n.k

4. Kipindi cha upasuaji
-Inapotokea kuna upasuaji mkubwa au wa dhararu basi mgonjwa atapaswa kutumia sindano ya Insulini kipindi hiki ili kuweza kudhibiti sukari kwa hali ya juu kwani kipindi hiki mwili huwa kwenye hali ya "stress"
-"Stress" inapelekea sukari kuongezeka na hata kuleta shida kuidhibiti kwa njia ya dawa za kumeza.
5. Kuibuka kwa madhara ya kisukari kwa mgonjwa
-Madhara ya kisukari hutokea haswa kwa sababu ya kutodhibiti sukari vizuri mwilini, madhara hayo ni pamoja na vidonda sugu katika miguu, figo kushindwa kufanya kazi n.k
-Inapotokea hali kama hizi zinazohitaji udhibiti imara wa sukari mwilini basi sindano ya Insulini itaanzishwa.
6. Mgonjwa mwenye kiwango cha sukari cha juu mno
-Kuna wagonjwa wanakutwa na kiwango kikubwa cha sukari kuanzia milimol kwa lita 33.3 au mashine ya kupima sukari inasoma "high", hawa wanahitaji kuanzishwa sindano ya insulini ili kusaidia kwa urahisi kushusha sukari. Hali hii inaweza kuchangiwa na maambukizi ya vimelea mwilini au hata kutokutumia dawa za kisukari
-Viwango kama hivi vya sukari hupelekea wagonjwa wengine kupoteza hadi fahamu wakati kufikishwa hospitalini.

Matibabu ya ugonjwa wa kisukari yana lengo kuu ya kuidhibiti sukari katika kiwango cha kawaida katika damu na dawa (sindano) ya insulini ni moja ya tiba bora kwa ugonjwa. Tafiti nyingi zimeonesha ufanisi mkubwa wa dawa ya `insulini katika udhibiti wa sukari mwili. Hakuna haja ya kuoga kutumia dawa hii pale inapokuhitaji kutumia kwa manufaa ya afya yako.
Share:

BAADHI YA MADHARA YA DAWA (SINDANO) YA INSULINI YANAYOWEZA KUTOKEA KWA MGONJWA MWENYE KISUKARI.

 Sindano ya Insulini ni moja ya dawa muhimu sana katika matibabu ya ugonjwa wa kisukari. Sindano hii huanzishwa kutokana na sababu mbalimbali kulingana na daktari alivyofanya tathmini. Insulini kama dawa zingine nayo ina madhara kadhaa kipindi mtu anaitumia ingawa faida ya dawa ni nyingi kuliko madhara yake. Ni vema kujua madhara haya ili usipatwe na wasiwasi. 

1. Kushusha sukari katika damu kuliko kawaida.

-Hii ni hali hatari sana ambayo imekuwa ikijitokeza miongoni mwa wangonjwa wanaotumia insulini. Mambo mbalimbali yameweza kuchangia kwa tatizo hili ikiwemo kutumia dozi kubwa sana ya dawa, kufanya mazoezi magumu sana baada ya kutumia Insulini,  kutopata "snacks " katikati ya milo mikubwa n.k

-Ushukaji huu wa sukari zaidi kwenye damu hupelekea mgonjwa kupatwa na dalili kama kuchoka sana, kizunguzungu, kutokwa na jasho jingi, kutetemeka, kukosa umakini n.k

2. Kuvimba na kuwasha eneo la sindano.

-Uchomaji wa sindano ya insulini unaweza kupelekea mzio(allergy) katika eneo la mwili (ngozi) linalochomwa na hivyo kupatwa na hali ya muwasho, kuvimba na hali ya wekundu eneo hilo

-Hali hii huweza kutokea ndani ya muda mfupi baada ya kuchoma sindano na huisha taratibu, huweza kuchukua hadi wiki 1.

3. Kusinyaa au kuvimba kwa ngozi

-Endapo sindano ya Insulini huchomwa eneo moja kwa muda mrefu bila ya kubadili eneo jingine , hii hupelekea kwa mabadiliko ya ngozi ambayo ni kuvimba au kusinyaa kwa ngozi eneo hilo. 

-Hali husababisha muonekano mbaya wa ngozi ya mgonjwa. 

4. Kuongezeka uzito.

-Matumizi ya sindano kwa wagonjwa wengi yameonekana kupelekea ongezeko la uzito huku sababu kamili ya tatizo hili halijapata majibu ya moja kwa moja.

-Hivyo wagonjwa ambayo wako kwenye Insulini wanatakiwa kuongeza umakini katika kudhibiti uzito wao kupitia vyakula wanavyokula na mazoezi.

5. Mzio (Allergy) wa mwili mzima

-Hali hii si rahisi na kawaida kutokea ingawa inaweza kutokea. Endapo inatokea hupelekea hali mbaya  sana na kusababisha dalili mbalimbali kwa mgojwa kama kupumua kwa shida, kutoka jasho kwa wingi, kuhisi kupoteza fahamu, mapigo ya moyo kwenda harakaharaka n.k

-Ikitokea hali hii inabidi ukimbizwe katika kituo cha afya cha karibu kwa matibabu ya haraka.

Ni muhimu sana kufuata maelekezo ya daktari kuhusiana na dawa ya Insulini lakini pia inashauriwa kuonana na daktari au mtaaalmu wa afya unapopatwa na shida au wasiwasi wowote katika utumiaji wa sindano ya Insulini.


Share:

Popular Posts

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Translate/tafsiri

Kunihusu

Picha yangu
KUWA MWENYE AFYA BORA NI JAMBO LA MSINGI SANA.BINAFSI ILI KUPATA MATOKEO MAZURI NAJITAHIDI KULA MLO KAMILI,KUFANYA MAZOEZI KILA SIKU ANGALAU KWA MUDA WA DAKIKA 30 NA PIA KUJENGA MUDA WA KUTOSHA KUUPUMZISHA MWILI BY DR FRANK

Lebo

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.